Jane's Journey

Home » Casts » Mzee Yusuf


Mzee Yusuf

Other Name/s: Mzee Yusuf a.k.a Mfalme

Actor | Singer | Song Writter

Mwimbaji na Mkurugenzi wa Jahazi Modern Taarab, Mzee Yusuf, amezaliwa Zanzibar mwaka 1977 na amemaliza darasa la 10 katika Shule ya Haile Selasie,

Mzee Yusuf 'Mfalme'

SWALI: Sasa turudi upande wa historia yako, labda tueleze ulizaliwa lini ukakulia wapi, maisha yako kwa ujumla.

JIBU: Nimezaliwa miaka 1977 na nimezaliwa Zanzibar. Nimelelewa kulekule nimekulia kulekule na kazi zangu nilianza kule kule za usanii, na nimemaliza darasa la 10 Zanzibar katika shule ya Haile Selasie.

Sikuwa nataka tena kuendelea na shule sababu niliona hali ngumu, si unajua maisha? nkaona hata! Hii ndio itanipeleka hii, sa niache huku. Niache moja nikamate moja.

Kwa hiyo niliacha shule, sikuendelea darasa la kumi na moja. Nikaanza mziki. Nilikuwa nafanya mziki nafanya maigizo, niko na shule, sa ilifika pahali sa nikachukuliwa na bendi ya melody.

Sa nkaona kidogo hapa kuna maslahi japo nilikuwa ‘napigwa buku kwa siku’ (nalipwa shilingi elfu moja kwa siku), lakini nilikuwa nashukuru sababu nilikuwa siipati ile buku,

SWALI: Sasa umeingia katika mziki wa taarabu. Ni muziki ambao kwa kweli unapendwa. Wengi wakisema mziki wa mwambao, wengine hivi, alimradi kila mtu na lugha yake anavyouita mziki huu. Ulipata ushawishi gani mpaka ukaingia katika ulimwengu huu wa mziki wa taarabu?

JIBU: Kwa kweli labda unajua kwa nilipokuwepo taarabu ndio ilikuwa inapendwa na nilikuwa na uwezo wa kuimba taarabu si vingine.

Na sikutegemea kama mtakuwa labda nami naweza kutunga nini mm’kh! Nilikuwa nahisi naweza kuimba. Sababu hata tulikuwa tunakaa nyumbani, tulikuwa tunamsikiliza mother (mama) anaimba, anaimba taarabu, tunakaa naye anatufahamisha hii inaimbwa hivi, hii ndio hivi, hii ndio hivi.

Sa ikafika mahali yani ile muziki ukawa unanijaa. Unanijaa sana kiasi ikafika mahala kwenye mazoezi ya mpira nawaambia wenzangu mimi ntakuwa naimba taarabu.

Basi kwa sababu nilikuwa napenda, halafu ni kwamba uwezo nilikuwa nao. Pale ndo nilipokuwa na ilo nivutia, lakini sio kuwa nilifikiria labda kumuona mtu mmmhkh! Sababu nilikuwa naweza.

Halafu mama yangu mzazi mwimbaji wa taarabu.

Filmography / Discography


External Links

  • Facebook Page of Mzee Yusuf
  • Twitter Page of Mzee Yusuf
  • YouTube of Mzee Yusuf
  • Website of Mzee Yusuf
 

More Photos

 
 
 

ABOUT US

BongoCinema.com is a one-stop online shop offering a huge variety of Bongo Movies on DVDs and Videos from Tanzania ...

Read More

HELP CENTRE and FAQ

# How do I make an order? # How long will it take to receive my order? # What Payment Options do I have? # Cancel my order? ...

Read More

Our Products

Action; Adventure; Comedy; Crime; Documentary; Drama; Educational; Family; Fantasy; History; Horror; Musical; Romance; Spiritual...

Read More

Comments /Maoni

John said, "I think I saw one of those bongo movie … you know those movies of the week. ... toa maoni yako kwenye bongo movie...

Read More